Kuhamisha Waasiliani kwa Kutumia Epson Device Admin

Hifadhi maelezo ya waasiliani kwenye faili.

Unaweza kuhariri faili zilizohifadhiwa katika umbizo wa SYLK au umbizo wa CSV kwa kutumia programu ya lahajedwali au kihariri cha matini. Unaweza kusajili yote pamoja baada ya kufuta au kuongeza maelezo.

Maelezo yanayojumuisha vipengee vya usalama kama vile nenosiri na maelezo ya kibinafsi yanaweza kuhifadhiwa katika umbizo wa njia mbili kwa nenosiri. Huwezi kuhariri faili hiyo. Hii inaweza kutumika kama faili chelezo ya maelezo ikijumuisha vipengele vya usalama.

  1. Anzisha Epson Device Admin.

  2. Teua Devices kwenye menyu ya kazi ya mwambaa.

  3. Teua kifaa ambacho unataka kusanidi kutoka kwa orodha ya kifaa.

  4. Bofya Device Configuration kwenye kichupo cha Home kwenye menyu ya riboni.

    Wakati nenosiri la msimamizi limewekwa, ingiza nenosiri kisha ubofye OK.

  5. Bofya Common > Contacts.

  6. Teua umbizo wa kuhamishwa kutoka kwenye Export > Export items.

    • All Items
      Hamisha faili ya njia mbili iliyosimbwa. Teua wakati ambapo unataka kujumuisha vipengee vya usalama kama vile nenosiri na maelezo ya kibinafsi. Huwezi kuhariri faili hiyo. Ukiiteua, ni lazima uweke upya nenosiri. Bofya Configuration na uweke nenosiri lenye vibambo kati ya urefu wa 8 na 63 katika ASCII. Nenosiri hili linahitajika unapoleya faili ya uwili.
    • Items except Security Information
      Hamisha faili zenye umbizo wa SYLK au umbizo wa CSV. Teua wakati ambapo unataka kuhariri maelezo ya faili iliyohamishwa.
  7. Bofya Export.

  8. Bainisha mahali pa kuhifadhi faili, teua aina ya faili, na kisha kubofya Save.

    Ujumbe wa kukamilisha unaonyeshwa.

  9. Bofya OK.

    Angalia kwamba faili imehifadhiwa kwenye mahali palipotajwa.