Kusajili Ufiko kwa Waasiliani kutoka kwa Paneli Dhibiti ya Kichapishi.

  1. Teua menyu kwenye paneli dhibiti ya kichapishi kama ilivyofafanuliwa hapa chini.

    Mipangilio > Kisimamia Waasiliani

  2. Teua Ongeza/Hariri/Futa.

  3. Fanya moja kati ya zifuatazo.

    • Ili kusajili mwasiliani mpya, teua kichupo cha Ongeza Mpya, na kisha uteue Ongeza Mwasiliani.
    • Ili kuhariri mwasiliani, teua mwasiliani anayelengwa, na kisha uteue Hariri.
    • Ili kufuta mwasiliani, teua mwasiliani anayelengwa, teua Futa, na kisha uteue Ndiyo. Hufai kutekeleza utaratibu unaofuata.
  4. Chagua aina ya ufikio kutoka kwa chaguo zinazoonyeshwa.

    Kumbuka:

    Huwezi kubadilisha aina baada ya kukamilisha usajili. Iwapo unataka kubadilisha aina, futa ufikio na usajili tena.

  5. Teua idadi unayotaka kusajili kama Nambari ya Usajili.

  6. Ingiza Jina na Neno la Kiolesura.

  7. Ingiza thamani kwa kila kipengee kinachosalia.

  8. Teua Sawa ili kutekeleza mipangilio.