Kusajili Ufiko kwa Wasiliani kutoka kwa Paneli Dhibiti ya Kichapishi (Wakati Bodi za Hiari za Faksi Zimesakinishwa)

Unaposajili mpokeaji kwenye orodha ya waasiliani, unaweza pia kuongeza mpangilio wa laini.

  1. Teua menyu kwenye paneli dhibiti ya kichapishi kama ilivyofafanuliwa hapa chini.

    Mipangilio > Kisimamia Waasiliani

  2. Teua Ongeza/Hariri/Futa.

  3. Fanya moja kati ya zifuatazo.

    • Ili kusajili mwasiliani mpya, teua kichupo cha Ongeza Mpya, na kisha uteue Ongeza Mwasiliani.
    • Ili kuhariri mwasiliani, teua mwasiliani anayelengwa, na kisha uteue Hariri.
    • Ili kufuta mwasiliani, teua mwasiliani anayelengwa, teua Futa, na kisha uteue Ndiyo. Hufai kutekeleza utaratibu unaofuata.
  4. Teua Faksi kutoka kwa chaguo za aina zilizoonyeshwa.

    Kumbuka:

    Huwezi kubadilisha aina baada ya kukamilisha usajili. Iwapo unataka kubadilisha aina, futa ufikio na usajili tena.

  5. Teua Nambari ya Faksi (Inahitajika).

  6. Chagua laini kwenye Ch. Mstari, kisha uteue Funga.

  7. Ingiza ufikio.

  8. Teua Sawa ili kutekeleza mipangilio.