Web Config ni programu ambayo huendeshwa katika kivinjari cha wavuti, kama vile Microsoft Edge na Safari, kwenye kompyuta na kifaa mahiri. Unaweza kuthibitisha hali ya printa au kubadilisha huduma ya ntandao na mipangilio ya printa. Ili utumie Web Config, unganisha printa na kompyuta au kifaa kwenye mtandao mmoja.
Vivinjari vifuatavyo vinakubaliwa. Tumia toleo jipya.
Microsoft Edge, Firefox, Chrome, Safari
Huenda ukaombwa kuingiza nenosiri la msimamzi unapoendesha Web Config. Tazama taarifa husika hapa chini ili kupata maelezo.