Kufungua Akaunti ya Mtumiaji

Fungua akaunti ya mtumiaji kwa ajili ya udhibiti wa ufikiaji.

  1. Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.

    Ingiza anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.

    Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.

    Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > (Wastani) > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi

  2. Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.

  3. Teua kwenye orodha inayofuata.

    Kichupo cha Product Security > Access Control Settings > User Settings

  4. Bofya Add kwa ajili ya nambari unayotaka kusajili.

    Muhimu:

    Unapotumia kichapishi na mfumo wa uhalalishaji wa Epson au makampuni mengine, sajili jina la mtumiaji la mpangilio wa uzuiaji katika nambari 2 hadi nambari 10.

    Programu kama vile mfumo wa uhalalishaji hutumia nambari moja, ili jina la mtumiaji lisionyeshwe kwenye paneli dhibiti ya kichapishi.

  5. Teua kila kipengee.

    • User Name:
      Ingiza jina la kuonyesha kwenye orodha ya jina la mtumiaji kwa urefu wa kati ya vibambo 1 na 14 ukitumia vibambo vya nambari.
    • Password:
      Ingiza nenosiri lenye vibambo kati ya urefu wa 0 na 70 katika ASCII (0x20 hadi 0x7E). Unapoanzisha nenosiri, liache tupu.
    • Select the check box to enable or disable each function.
      Teua kipengele unachotaka kutumia.
      Iwapo utateua Print from Computer kwenye Allow only B&W printing, kichapishi hakitakubali uchapishaji wa rangi kutoka kwenye kompyuta.
  6. Bofya Apply.

    Rejesha mipangilio ya orodha ya mtumiaji baada ya kipindi maalum cha muda.

    Hakikisha kwamba jina la mtumiaji ulilosajili kwenye User Name limeonyeshwa na kubadilisha Add hadi Edit.

    Msimamizi anayesanidi udhibiti wa ufikiaji wataarifu mtumiaji wa maelezo ya akaunti na kiwango cha utendaji unaopatikana.