Kusanidi Mipangilio Msingi ya SSL/TLS

Iwapo kichapishi kinatumia kipengele cha seva cha HTTPS, unaweza kutumia mawasiliano ya SSL/TLS kusimba mawasiliano. Unaweza kusanidi na kudhibiti kichapishi ukitumia Web Config huku ukihakikisha usalama.

Sanidi uthabiti uliosimbwa kwa njia fiche na kipengele cha kuelekeza upya.

  1. Fikia Web Config na uteue kichupo cha Network Security > SSL/TLS > Basic.

  2. Teua thamani kwa kila kipengee.

    • Encryption Strength
      Teua kiwango cha uthabiti wa usimbaji kwa njia fiche.
    • Redirect HTTP to HTTPS
      Elekezea upya kwenye HTTPS wakati HTTP ikifikiwa.
  3. Bofya Next.

    Ujumbe wa uthibitishaji unaonyeshwa.

  4. Bofya OK.

    Kichapishi kimesasishwa.