Unaweza kubainisha wapokeaji kwenye kichupo cha Mpokeaji ili kutuma faksi kwa kutumia mbinu zifuatazo.
Teua Kibodi, ingiza nambari ya faksi kwenye skrini inayoonyeshwa, na kisha udonoe Sawa.
- Ili kuongeza kusitisha (sitisha kwa sekunde tatu wakati wa kupiga) ingiza kistari kifupi (-).
- Ikiwa utaweka msimbo wa ufikiaji wa nje katika Aina ya Laini, ingiza “#” (hashi) badala ya msimbo wa ufikiaji wa nje mwanzoni wa nambari ya faksi.
Iwapo huwezi kuingiza nambari ya faksi kikuli, Vikwazo vya Kupiga Moja kwa moja kwenye Mipangilio ya Usalama imewekwa kwa On. Teua wapokeaji wa faksi kutoka kwenye orodha ya waasiliani au historia ya faksi iliyotumwa.
Teua Waasiliani na uteue wapokeaji unaotaka kutuma. Iwapo bado mpokeaji unayetaka kumtumia hajasajiliwa kwenye Waasiliani, donoa
ili kuisajili.
Teua Hivi karibuni, na kisha uteue mpokeaji.
Teua mpokeaji kutoka kwenye orodha iliyosajiliwa katika Mipangilio > Kisimamia Waasiliani > Mara kwa mara.
Ili kufuta wapokeaji uliowaingiza, onyesha orodha ya wapokeaji kwa kudonoa sehemu kwenye skrini ambayo inaonyesha nambari ya faksi au iidadi ya wapokeaji kwenye skrini ya LCD, teua mpokeaji kutoka kwenye orodha, na kisha uteue Ondoa.