Unapounganisha kompyuta kwenye kichapishi kwa kutumia WSD, fuata hatua hapa chini ili kuendesha Web Config.
Fungua orodha ya vichapishi kwenye kompyuta.
Bofya kulia kwenye kichapishi chako na uteue Sifa.
Teua kichupo cha Huduma ya Wavuti na ubofye URL.
Kwa vile kichapishi kinatumia cheti cha kutiwa sahihi binafsi kufikia HTTPS, onyo huonyeshwa kwenye kivinjari unapoanza Web Config; hii haionyeshi kuwa kuna tatizo na unaweza kupuuza kwa usalama.