Mifano ya Usanidi wa IPsec/IP Filtering

Kupokea pakiti za IPsec pekee

Mfano huu ni wa kusanidi sera chaguomsingi pekee.

Default Policy:

  • IPsec/IP Filtering: Enable

  • Access Control: IPsec

  • Authentication Method: Pre-Shared Key

  • Pre-Shared Key: ingiza hadi vibambo 127.

Group Policy: usisanidi.

Kupokea data ya kuchapisha na mipangilio ya kichapishi

Mfano huu huruhusu mawasiliano ya data ya uchapishaji na usanidi wa kichapishi kutoka huduma zilizobainishwa.

Default Policy:

  • IPsec/IP Filtering: Enable

  • Access Control: Refuse Access

Group Policy:

  • Enable this Group Policy: teua kisanduku.

  • Access Control: Permit Access

  • Remote Address(Host): anwani ya IP ya kiteja

  • Method of Choosing Port: Service Name

  • Service Name: teua kisanduku cha ENPC, SNMP, HTTP (Local), HTTPS (Local) na RAW (Port9100).

Kumbuka:

Ili kuepuka kupokea HTTP (Local) na HTTPS (Local), futa visanduku vyao vya kuteua kwenye Group Policy. Unapofanya hivyo, lemaza uchujaji wa IPsec/IP kutoka kwenye paneli dhibiti ya kichapishi kwa muda ili kubadilisha mipangilio ya kichapishi.

Kupokea ufikiaji kutoka anwani ya IP iliyobainishwa pekee

Mfano huu huruhusu anwani ya IP iliyobainishwa kufikia kichapishi.

Default Policy:

  • IPsec/IP Filtering: Enable

  • Access Control:Refuse Access

Group Policy:

  • Enable this Group Policy: teua kisanduku.

  • Access Control: Permit Access

  • Remote Address(Host): anwani ya IP ya mteja wa msimamizi

Kumbuka:

Licha ya sera za usanidi, mteja ataweza kufikia na kusanidi kichapishi.