> Maelezo ya Msimamizi > Mipangilio Mahiri ya Usalama > Kudhibiti Kutumia Itifaki > Itifaki unazoweza Kuwezesha au Kulemaza

Itifaki unazoweza Kuwezesha au Kulemaza

Itifaki

Ufafanuzi

Bonjour Settings

Unaweza kubainisha iwapo utatumia Bonjour. Bonjour inatumiwa kutafuta vifaa, chapisho, nakadhalika.

SLP Settings

Unaweza kuwezesha au kulemaza kitendaji cha SLP. SLP inatumika kwa utambazaji wa kusukuma na utafutaji wa mtandao kwenye EpsonNet Config.

WSD Settings

Unaweza kuwezesha au kulemaza kitendaji cha WSD. Hii inapowezeshwa, unaweza kuongeza vifaa vya WSD, na uchapishe kutoka kwenye kituo tayarishi cha WSD.

LLTD Settings

Unaweza kuwezesha au kulemaza kitendaji cha LLTD. Hii inapowezeshwa, inaonyeshwa kwenye ramani ya mtandao wa Windows.

LLMNR Settings

Unaweza kuwezesha au kulemaza kitendaji cha LLMNR. Hii inapowezeshwa, unaweza kutumia mwonekano wa jina bila NetBIOS hata iwapo huwezi kutumia DNS.

LPR Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu uchapishaji wa LPR au la. Hii inapowezeshwa, unaweza kuchapisha kutoka kituo cha LPR.

RAW(Port9100) Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu uchapishaji kutoka kituo cha RAW au la (Kituo cha 9100). Hii inapowezeshwa, unaweza kuchapisha kutoka kituo cha RAW (Kituo cha 9100).

IPP Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu uchapishaji kutoka IPP au la. Hii inapowezeshwa, unaweza kuchapisha kupitia Mtandao.

FTP Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu uchapishaji wa FTP au la. Hii inapowezeshwa, unaweza kuchapisha kupitia seva ya FTP.

SNMPv1/v2c Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu SNMPv1/v2c au la. Hii inatumika kusanidi vifaa, kufuatilia, na kadhalika.

SNMPv3 Settings

Unaweza kubainisha iwapo utaruhusu SNMPv3 au la. Hii inatumika kusanidi vifaa vilivyosimbwa fiche, kufuatilia, nk.