> Utambazaji > Kutambaza Nakala Asili kwenye Kompyuta > Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Unaweza kuhifadhi picha zilizochanganuliwa kwenye kompyuta iliyounganishwa kwenye kichapishi kupitia kebo ya USB.

Kumbuka:

Ili kutumia kipengele hiki, hakikisha kwamba programu zifuatazo zimesakinishwa kwenye kompyuta yako.

  • Epson ScanSmart (Windows 7 au la naadaye, au OS X El Capitan au la baadaye)

  • Epson Event Manager (Windows Vista/Windows XP, au OS X Yosemite/OS X Mavericks/OS X Mountain Lion/Mac OS X v10.7.x/Mac OS X v10.6.8)

  • Epson Scan 2 (programu zinazohitajika ili utumie kipengele cha kitambazaji)

Tazama yafuatayo ili uangalie ikiwa kuna programu za kusakinisha.

Windows 10: bofya kitufe cha kuwasha, na kisha ukague kabrasha la Epson Software > Epson ScanSmart, na kabrasha la EPSON > Epson Scan 2.

Windows 8.1/Windows 8: andika jina la programu katika sehemu ya utafutaji, na kisha uchague ikoni inayoonekana.

Windows 7: bofya kitufe cha kuwasha kisha uteue Programu Zote. Ifuatayo, angalia kabrasha la Epson Software > Epson ScanSmart, na kabrasha la EPSON > Epson Scan 2.

Windows Vista/Windows XP: bofya kitufe cha kuwasha kisha uteue Programu Zote au Programu. Ifuatayo, angalia kabrasha la Epson Software > Epson Event Manager, na kabrasha la EPSON > Epson Scan 2.

Mac OS: teua Nenda > Programu > Epson Software.

  1. Weka nakala za kwanza.

    Kuweka Nakala Asili kwenye Glasi ya Kichanganuzi

  2. Bonyeza kitufe cha na kitufe cha kwa wakati mmoja ili kuanza kuchanganua.

    Unapotumia Windows 7 au la baadaye, au OS X El Capitan au la baadaye: Epson ScanSmart huwashwa kiotomatiki kwenye kompyuta yako, na utambazaji huanza.

    Kumbuka:
    • Tazama usaidizi wa Epson ScanSmart kwa taarifa kamili ya kutumia programu. Bofya Help kwenye skrini ya Epson ScanSmart ili kufungua msaada.

    • Unaweza kuanza kutambaza sio tu kutoka kwenye kichapishi bali pia kutoka kwenye kompyuta yako kwa kutumia Epson ScanSmart.