Haiwezi Kutuma Faksi kwa Mpokeaji Fulani

Sababu zifuatazo zinaweza kuzingatiwa.

Mashine ya mpokeaji inachukua muda mrefu kabla ya kujibu.

Suluhisho

Ikiwa mashine ya mpokeaji haichukui simu yako ndani ya sekunde 50 baada ya printa kimaliza kudayo, simu hiyo itakatika kwa hitilafu. Dayo ukitumia simu iliyounganishwa ili ukague muda inayochukua kabla ya kusikia toni ya faksi. Ikiwa itachukua zaidi ya sekunde 50, ongeza kusimamisha bada ya nambari ya faksi ili utume faksi. Inatumiwa kuingiza usitishaji. Kistari kinaingizwa kama alama ya kusimamisha. Kusimamisha mara moja ni kama sekunde tatu. Ongeza kusimamisha mara nyingi inavyohitajika.

Mpangilio wa Kasi ya Faksi uliosajiliwa kwenye orodha ya waasiliani sio sahihi.

Suluhisho

Teua Mipangilio > Kisimamia Waasiliani > Hariri, na kisha uteue mpokeaji kutoka kwenye orodha ya waasiliani. Fuata maagizo kwenye skrini, na kisha uteue Modi ya Mawasiliano kuwa Polepole(9,600bps).