Kuunda Mipangilio ya Wi-Fi kwa Kuingiza SSID na Nenosiri

Unaweza kusanidi mtandao wa Wi-Fi kwa kuingiza maelezo muhimu ya kuunganisha kwenye kipanga njia pasiwaya kutoka kwenye paneli dhibiti ya kichapishi. Ili kusanidi kwa kutumia mbinu hii, unahitaji SSID na nenosiri kwa kipanga njia pasiwaya.

Kumbuka:

Iwapo unatumia kipamnga njia pasiwaya na mipangilio chaguo-msingi, SSID na nenosiri vipo kwenye lebo. Iwapo hujui SSID na nenosiri, wasiliana na mtu aliyesanidi kipanga njia pasiwaya, au tazama uwekaji nyaraka uliotolewa na kipanga njia pasiwaya.

  1. Teua Usanidi wa Wi-Fi kwenye skrini ya nyumbani.

    Ili kuteua kipengee, tumia vitufe vya , na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

  2. Teua Wi-Fi (Inapendekezwa).

  3. Bonyeza kitufe cha OK ili kuendelea.

  4. Teua Kisogora cha Usanidi wa Wi-Fi.

  5. Teua SSID kwa kipanga njia pasiwaya kutoka kwenye paneli dhibiti ya kichapishi, na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

    Kumbuka:
    • Iwapo SSID unayotaka kuunganisha kwayo haionyeshwi kwenye paneli ya udhibiti ya kichapishi, bonyeza ili kusasisha orodha. Iwapo bado haitaonyeshwa, teua SSID nyingine, na kisha uingize SSID moja kwa moja.

    • Iwapo hujui SSID, angalia kama imeandikwa kwenye lebo ya kipanga njia pasiwaya. Iwapo unatumia kipanga njia pasiwaya kwa mipangilio chaguo-msingi, tumia SSID iliyoandikwa kwenye lebo.

  6. Ingiza nywila.

    Teua iwapo unachapisha ripoti ya muunganisho wa mtandao baada ya kukamilisha mipangilio au la.

    Kumbuka:
    • Nenosiri linaathiriwa na herufi kubwa au ndogo.

    • Iwapo hujui jina la mtandao (SSID) angalia iwapo maelezo yameandikwa kwenye lebo ya kipanga njia pasiwaya. Iwapo unatumia kipanga njia pasiwaya kwa mipangilio yake chaguo-msingi, tumia SSID kwenye lebo. Iwapo huwezi kutafuta maelezo yoyote, tazama nyaraka zilizotolewa pamoja na kipanga njia pasiwaya.

  7. Unapokamilisha usanidi, na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

    Kumbuka:

    Ukishindwa kuunganisha, pakia karatasi, na kisha ubonyeze kitufe cha ili kuchapisha ripoti ya muunganisho wa mtandao.