> Utambazaji > Kutambaza Nakala Asili kwenye Kompyuta > Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Kumbuka:

Ili kutumia kipengele hiki, hakikisha kwamba programu zifuatazo zimesakinishwa kwenye kompyuta yako.

  • Epson Event Manager

  • Epson Scan 2

Tazama yafuatayo ili uangalie ikiwa kuna programu za kusakinisha.

Windows 10: bofya kwenye kitufe cha kuwasha, na kisha uteue Mifumo ya WindowsPaneli DhibitiProgramuProgramu na Vipengele.

Windows 8.1/Windows 8: teua Eneo-KaziMipangilioPaneli DhibitiProgramuProgramu na Vipengele.

Windows 7: bofya kitufe cha kuwasha, na kisha uteue Paneli DhibitiProgramuProgramu na Vipengele

Mac OS: teua Nenda > Programu > Epson Software.

  1. Weka nakala za kwanza.

    Kuweka Nakala Asili kwenye Glasi ya Kitambazaji

  2. Teua Changanua kwenye paneli dhibiti.

    Ili kuteua kipengee, tumia vitufe vya , na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

  3. Teua jinsi ya kuhifadhi picha iliyotambazwa kwenye kompyuta kutoka kwenye menyu zifuatazo, na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

    • Kwenye Kompyuta (JPEG): huhifadhi picha iliyotambazwa kwenye umbizo la JPEG.
    • Kwenye Kompyuta (PDF): huhifadhi picha iliyotambazwa kwenye umbizo la PDF.
    • Kwenye Kompyuta (Barua pepe): huanzisha huduma ya barua pepe kwenye kompyuta, na kisha huiambatisha kiotomatiki kwenye barua pepe.
    • Kwenye Kompyuta (Maalum): huhifadhi picha iliyotambazwa kwa kutumia mipangilio kwenye Epson Event Manager. Unaweza kubadilisha mipangilio ya utambazaji kama vile ukubwa wa kutambaza, kabrasha la kuhifadhi, au umbizo la kuhifadhi.
  4. Teua kompyuta unayotaka kuhifadhi picha zilizotambazwa.

    Kumbuka:
    • Wakati kichapishi kimeunganishwa kwenye mtandao, unaweza kuteua kompyuta ipi ambayo unataka kuhifadhi taswira iliyotambazwa. Unaweza kuonyesha hadi kompyuta 20 kwenye paneli dhibiti ya kichapishi. Ukiweka Network Scan Name (Alphanumeric) katika Epson Event Manager, huonyeshwa kwenye paneli dhibiti.

  5. Bonyeza kitufe cha .