> Maelezo ya Msimamizi > Mipangilio ya Usalama wa Bidhaa > Kusimba Nenosiri kwa Njia fiche

Kusimba Nenosiri kwa Njia fiche

Kusimba nenosiri kwa njia fiche hukuruhusu kusimba maelezo ya siri (manenosiri yote, funguo za cheti cha faragha) yaliyohifadhiwa kwenye kichapishi.

  1. Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.

    Ingiza anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.

    Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.

    Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi

  2. Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.

  3. Teua kwenye orodha inayofuata.

    Kichupo cha Product Security > Password Encryption

    Kumbuka:

    Unaweza pia kuweka mipangilio kwenye paneli dhibiti ya kichapishi.

    Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Usimamizi wa Mtandao > Mipangilio ya Usalama > Ufichamishaji wa Nenosiri

  4. Teua ON ili kuwezesha usimbuaji.

  5. Bofya OK.