Kusanidi Sera ya Chaguo-msingi

Kuchuja trafiki, sanidi sera ya faragha. Sera ya chaguo-msingi inatumika na kila mtumiaji au kikundi kinachounganisha kwenye kichapishi. Kwa udhabidi zaidi wa kina kuhusu watumiaji na vikundi vya watumiaji, sanidi sera za kikundi.

  1. Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.

    Ingiza anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.

    Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.

    Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi

  2. Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.

  3. Teua kwenye orodha inayofuata.

    Kichupo cha Network Security > IPsec/IP Filtering > Basic

  4. Ingiza thamani kwa kila kipengee.

  5. Bofya Next.

    Ujumbe wa uthibitishaji unaonyeshwa.

  6. Bofya OK.

    Kichapishi kimesasishwa.