Kwa sababu Self-signed Certificate kinatolewa na kichapishi, unaweza kukisasisha wakati muda wake umekwisha au wakati maudhui yaliyofafanuliwa hubadilika.
Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.
Ingiza anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.
Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.
Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi
Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.
Teua kwenye orodha inayofuata.
Kichupo cha Network Security > SSL/TLS > Certificate
Bofya Update.
Ingiza Common Name.
Unaweza kuingiza anwani za 5 IPv4, anwani za IPv6, majina ya mpangishaji, FQDNs kati ya vibambo 1 hadi 128 na kuvitenganishwa kwa koma. Kigezo cha kwanza kinahifadhiwa kwenye jina la kawaida na vingine vinahifadhiwa kwenye sehemu mbadala kwa mada ya cheti.
Mfano:
Anwani ya IP ya kichapishi: 192.0.2.123, Jina la kichapishi: EPSONA1B2C3
Jina la kawaida: EPSONA1B2C3,EPSONA1B2C3.local,192.0.2.123
Bainisha kipindi cha uhalali cha cheti.
Bofya Next.
Ujumbe wa uthibitishaji unaonyeshwa.
Bofya OK.
Kichapishi kimesasishwa.
Unaweza kuangalia maelezo ya cheti kutoka katika kichupo cha Network Security > SSL/TLS > Certificate > Self-signed Certificate na ubofye Confirm.