> Maelezo ya Msimamizi > Kudhibiti Kichapishi > Kuweka Paneli Dhibiti

Kuweka Paneli Dhibiti

Usanidi wa paneli dhibiti ya kichapishi. Unaweza kusanidi kama ifuatavyo.

  1. Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.

    Ingiza anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.

    Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.

    Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi

  2. Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.

  3. Teua kwenye orodha inayofuata.

    Kichupo cha Device Management > Control Panel

  4. Weka vipengee vifuatavyo inavyohitajika.

    • Language
      Teua lugha iliyoonyeshwa kwenye paneli dhibiti.
    • Panel Lock
      Iwapo utateua ON, nenosiri la msimamizi linahitajika unapotekeleza operesheni inayohitaji mamlaka ya msimamizi. Iwapo nenosiri la msimamizi halijawekwa, kufuli la paneli limelemazwa.
    • Operation Timeout
      Iwapo utateua ON, unapoingia kama mtumiaji wa kudhibiti ufikiaji au msimamizi, unaondolewa kiotomatiki na kuenda kwenye skrini ya mwanzo iwapo hakuna shughuli kwa kipindi fulani cha muda.
      Unaweza kuweka kati ya sekunde 10 na dakika 240 kulingana na sekunde.
    Kumbuka:

    Unaweza pia kuweka mipangilio kwenye paneli dhibiti ya kichapishi.

    • Language: Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio Msingi > Lugha/Language

    • Panel Lock: Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Usimamizi wa Mtandao > Mipangilio ya Usalama > Mipangilio ya Msimamizi > Mpangilio wa Kufunga

    • Operation Timeout: Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio Msingi > Muda wa Shughuli Umeisha (Unaweza kubainisha Kuwasha au Kuzima).

  5. Bofya OK.