> Utambazaji > Kutambaza Nakala Asili kwenye Kompyuta > Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Kutambaza Kutoka kwa Paneli Dhibiti

Kumbuka:

Ili kutumia kipengele hiki, hakikisha kwamba programu zifuatazo zimesakinishwa kwenye kompyuta yako.

  • Epson Event Manager

  • Epson Scan 2

Tazama yafuatayo ili uangalie ikiwa kuna programu za kusakinisha.

/Windows 10: Bofya kiungo cha kuwasha kisha uchague Mifumo ya WindowsPaneli DhibitiProgramuProgramu na Vipengele.

/Windows 8.1/Windows 8: Chagua Eneo-KaziMipangilioPaneli DhibitiProgramuProgramu na Vipengele.

/Windows 7: Bofya kitufe cha kuwasha kisha uteue, Paneli DhibitiProgramu-Programs and Features

Mac OS: Teua Nenda > Programu > Epson Software.

  1. Weka nakala za kwanza.

    Kuweka nakala Asili kwenye glasi ya kichanganuzi

  2. Teua Scan kwenye paneli dhibiti.

  3. Teua Computer.

  4. Chagua kompyuta ya kuhifadhi picha zilizochanganuliwa.

    • Ikiwa skrini ya Select Computer imeonyeshwa, teua kompyuta kutoka kwenye skrini.
    • Iwapo skrini ya Scan to Computer imeonyeshwa na kompyuta tayari imeteuliwa, hakikisha kompyuta iliyoteuliwa ni sahihi. Iwapo unataka kubadilisha kompyuta, teua , kisha uteue kompyuta nyingine.
    Kumbuka:
    • Wakati kichapishi kimeunganishwa kwenye mtandao, unaweza kuteua kompyuta ipi ambayo unataka kuhifadhi taswira iliyotambazwa. Unaweza kuonyesha hadi kompyuta 20 kwenye paneli dhibiti ya kichapishi. Ukiweka Network Scan Name (Alphanumeric) katika Epson Event Manager, huonyeshwa kwenye paneli dhibiti.

  5. Teua ili kuteua jinsi ya kuhifadhi picha iliyotambazwa kwenye kompyuta.

    • Save as JPEG: Huhifadhi picha iliyotambazwa kwenye umbizo la JPEG.
    • Save as PDF: Huhifadhi picha iliyotambazwa kwenye umbizo la PDF.
    • Attach to e-mail: Huanzisha huduma ya barua pepe kwenye kompyuta, na kisha huiambatisha kiotomatiki kwenye barua pepe.
    • Follow custom setting: Huhifadhi picha iliyotambazwa kwa kutumia mipangilio kwenye Epson Event Manager. Unaweza kubadilisha mipangilio ya utambazaji kama vile ukubwa wa kutambaza, kabrasha la kuhifadhi, au umbizo la kuhifadhi.
  6. Donoa .

Kumbuka:

Rangi, ukubwa, na ukingo wa taswira iliyotambazwa hautakuwa sawa na asili.