Unaweza kuchapisha kutumia njia na itifaki anuwai.
Iwapo unatumia kichapishi chenye kazi anuwai, unaweza kutumia utambazaji wa mtandao na PC-FAX kutoka kwa nambari isiyobainishwa ya kompyuta za mtandao.
Unaweza kupunguza hatari za usalama zisizotarajiwa kwa kuzuia uchapishaji kutoka kwa njia maalum au kudhibiti kazi zinazopatikana.
Fuata hatua zilizo hapa chini ili kusanidi mipangilio ya itifaki.
Weka anwani ya IP ya kichapishi katika kivinjari ili kufikia Web Config.
Ingiza anwani ya IP ya mtandao (kamili/wa ziada) ambao unataka kusanidi kutoka kwa kompyuta ambayo imeunganishwa kwenye mtandao sawa na wa kichapishi.
Unaweza kuangalia anwani ya IP ya kichapishi kutoka kwa menyu inayofuata.
Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Mtandao > (Wastani au Ya Ziada) > Hali ya Mtandao > Hali ya LAN ya waya/Wi-Fi
Ingiza nenosiri la msimamizi ili kuingia kama msimamizi.
Teua kwenye orodha inayofuata.
Kichupo cha Network Security > Protocol
Sanidi kila kipengee.
Bofya Next.
Bofya OK.
Mipangilio inatumika kwenye kichapishi.