Kuhifadhi Vikundi vya Kunakili

  1. Teua Nakili kwenye paneli dhibiti ya kichapishi.

  2. Teua kichupo cha Mahiri, na kisha uteue Seti za Chapisho.

  3. Teua Haijawekwa kutoka kwenye orodha, na kisha uteue Sajili/Futa.

  4. Ingiza jina la kikundi.

  5. Bainisha nakala na seti kwenye kichupo cha Nakala na Seti.

    Kwa mfano, iwapo ulitaka kuchapisha vijitabu vya madarasa manne (Darasa la 1: wanafunzi 30, Darasa la 2: wanafunzi 31, Darasa la 3: wanafunzi 32, Darasa la 4: wanafunzi 30) kwa shule, utaweka mipangilio ifuatayo.

  6. Teua laha za slipu na uondoe mipangilio ya karatasi kwenye kichupo cha Kumalizia.

  7. Teua Sawa ili kuhifadhi.