Mipangilio ya Faksi

Teua menyu kwenye paneli dhibiti kama ilivyofafanuliwa hapa chini.

Faksi > Mipangilio ya Faksi

Mipangilio ya Utambazaji:
Ukubwa Asili (Glasi):

Teua ukubwa na uelekeo wa waraka halisi uliyowekwa kwenye glasi ya kichanganuzi.

Aina Asili:

Teua aina ya nakala yako asili.

Hali ya Rangi:

Teua iwapo utatambaza kwenye rangi au katika monokromu.

Mwonekano:

Teua mwonekano wa faksi inayotoka. Iwapo utateua mwonekano wa juu, ukubwa wa data unakuwa mkubwa na inachukua muda ili kutuma faksi.

Uzito:

Huweka uzito wa faksi inayotoka. + hufanya uzito kolevu zaidi, na - huufanya mwepesi.

Ondoa Mand'yuma:

Teua ukolevu wa mandharinyuma. Donoa + ili kuongeza mwangaza (weupe) kwenye mandharinyuma na udonoe - ili kuikoleza (kuongeza weusi).

Iwapo utateua Otomatiki, rangi za mandharinyuma za nakala asili zimetambuliwa, na zinaondolewa au kufifishwa kiotomatiki. Haitekelezwi sahihi iwapo rangi ya mandharinyuma ni kolevu zaidi au haijatambulika.

Ukali:

Huboresha au kuondoa ulengaji wa muhtasari wa taswira. + huboresha kali, na - huondoa ulengaji wa ukali.

ADF Pande 2:

Huchanganua pande zote za hati halisi zilizowekwa katika ADF na kutuma faksi ya rangi moja.

Uta'ji Unao'a ADF:

Wakati unatuma faksi kutoka kwenye ADF, huwezi kuongeza hati halisi katika ADF, baada ya kuanzisha uchanganuzi. Ukiweka hati halisi zenye ukubwa tofauti katika ADF, hati zote halisi hutumwa kwa ukubwa wa juu zaidi kati ya hizo. Wezesha chaguo hili ili printa ikuulize ikiwa unataka kuchanganua ukurasa mwingine baada ya hati halisi katika ADF imemaliza kuchanganua. Kisha unaweza kuchambua na kuchanganua hati zako halisi kwa ukubwa na kuzituma kama faksi moja.

Mipangilio ya Kutuma Faksi:
Tuma Moja kwa Moja:

Hutuma faksi ya rangi moja inapotambaza nakala asili. Kwa kuwa nakala asili zilizotambazwa hazihifadhiwi kwa muda kwenye kumbukumbu ya kichapishi hata wakati wa kutuma kiwango kikubwa cha kurasa, unaweza kuzuia makosa ya kichapishi kwa sababu ya kutokuwa na kumbukumbu. Kumbuka kuwa kutuma kwa kutumia kipengele hiki huchukua muda mrefu kuliko kutotumia kipengele hiki. Tazama maelezo husiani hapa chini kuhusu mada hii.

Huwezi kutumia kipengee hiki wakati:

  • Kutuma faksi kwa kutumia chaguo la ADF Pande 2

  • Kutuma faksi kwa wapokeaji wengi

Kipaumbele cha Kutuma:

Hutuma faksi ya sasa kabla ya faksi nyingine zinazosubiri kutumwa. Tazama maelezo husiani hapa chini kuhusu mada hii.

Tuma Faksi Baadaye:

Hutuma faksi wakati ambao ulibainisha. Faksi ya rangi moja tu ndio inayopatikana wakati unatumia chaguo hili. Tazama maelezo husiani hapa chini kuhusu mada hii.

Ongeza Maelezo ya Mtumaji:
  • Ongeza Maelezo ya Mtumaji

    Teua eneo ambalo unataka kujumuisha maelezo ya kijajuu (jina la mtumaji na nambari ya faksi) kwenye faksi inayoondoka, au kutojumuisha maelezo.

    - Zima: hutuma faksi isiyokuwa na maelezo ya kijajuu.

    - Nje ya Picha: hutuma faksi pamoja na maelezo ya kijajuu katika pambizo nyeupe ya juu ya faksi. Hii huzuia kijajuu kupitana na taswira iliyotambazwa, hata hivyo,faksi iliyopokewa na mpokeaji inaweza kuchapishwa katika laha mbili kulingana na ukubwa wa nakala asili.

    - Ndani ya Picha: hutuma faksi kwa maelezo ya kijajuu karibu 7 mm chini kuliko upande wa juu wa taswira iliyotambazwa. Kijajuu kinaweza kupitana na taswira, hata hivyo, faksi iliyopokewa na mpokeaji haitagawanywa kwa nyaraka mbili.

  • Kijajuu cha Faksi

    Teua kijajuu kwa mpokeaji. Ili kutumia kipengele hiki, lazima usajili vijajuu anuwai mapema.

  • Maelezo ya Ziada

    Teua maelezo unayotaka kuongeza. Unaweza kuteua moja kutoka Nambari Yako ya Simu, Orodha ya Mfikio, na Hamna.

Niarifu kuhusu Matokeo ya Kutuma:

Hutuma taarifa baada ya kutuma faksi.

Ripoti ya Upitishaji:

Huchapisha ripoti ya usambazaji baada ya wewe kutuma faksi.

Chapisha Hitilafu Ikitokea huchapisha ripoti wakati kosa hutokea tu.

Wakati Ambatisha Taswira ya Faksi kwenye ripoti imewekwa kwenye Mipangilio > Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Faksi > Mipangilio ya Ripoti, faksi zilizo na makosa pia huchapisha pamoja na ripoti.

Chelezo:

Huhifadhi chelezo cha faksi iliyotumwa ambayo imetambazwa na kuhifadhiwa kwenye kumbukumbu ya kichapishi kiotomatiki. Kipengele cha chelezo kinapatikana wakati:

  • Kutuma faksi kwenye monokromu

  • Kutuma faksi kutumia kipengele cha Tuma Faksi Baadaye

  • Kutuma faksi kutumia kipengele cha Tuma Bechi

  • Kutuma faksi kutumia kipengele cha Hifadhi Data ya Faksi

Jina la Faili:

Iwapo utaweka hii iwe Washa na utume faksi, unaweza kubainisha jina la waraka la kuhifadhiwa kwenye kikasha cha Nyaraka Zilizohifadhiwa na kikasha cha Tuma Kura/Ubao.