Unaweza kusanidi mtandao wa Wi-Fi kwa kuingiza maelezo muhimu ya kuunganisha kwenye kipanga njia pasiwaya kutoka kwenye paneli dhibiti ya kichapishi. Ili kusanidi kwa kutumia mbinu hii, unahitaji SSID na nenosiri kwa kipanga njia pasiwaya.
Iwapo unatumia eneo la kipanga njia pasiwaya kwa mipangilio yake chaguo-msingi, SSID na nywila ziko kwenye lebo. Iwapo hufahamu SSID na nywila, tazama nyaraka zilizotolewa na kipanga njia pasiwaya.

Teua
kwenye skrini ya nyumbani.
Ili kuteua kipengee, tumia vitufe vya
, na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

Teua Wi-Fi (Inapendekezwa).
Bonyeza kitufe cha OK ili kuonyesha skrini inayofuata.
Iwapo tayari muunganisho wa mtandao umesanidiwa, maelezo ya muunganisho yanaonyeshwa. Teua Badilisha Mipangilio ili kubadilisha mipangilio.
Teua Sogora ya Kusanidi Wi-Fi.
Fuata maagizo yaliyo kwenye skrini ili kuteua SSID, weka nywila ya kipanga njia pasi waya na usanidi.
Ukitaka kuangalia hali ya muunganisho wa mtandao ya kichapishi baada ya kukamilisha kusanidi, angalia kiungo cha maelezo husiani kilicho hapa chini kwa maelezo.
Iwapo hujui SSID, angalia kama imeandikwa kwenye lebo ya kipanga njia pasiwaya. Iwapo unatumia kipanga njia pasiwaya kwa mipangilio chaguo-msingi, tumia SSID iliyoandikwa kwenye lebo. Iwapo huwezi kutafuta maelezo yoyote, tazama nyaraka zilizotolewa pamoja na kipanga njia pasiwaya.
Nenosiri linaathiriwa na herufi kubwa au ndogo.
Iwapo hujui nenosiri, angalia iwapo maelezo yameandikwa kwenye lebo ya kipanga njia pasiwaya. Kwenye lebo, nenosiri linaweza kuandikwa “Network Key”, “Wireless Password”, na kadhalika. Ikiwa unatumia kipanga njia pasiwaya na mipangilio yake chaguomsingi, tumia nenosiri lilioandikwa kwenye lebo.