Chagua Mipangilio kwenye skrini ya mwanzo kwenye paneli dhabiti ya kichapishi, na kisha uchague Mipangilio ya Jumla > Mipangilio ya Faksi > Sogora ya Mpangilio wa faksi.
Kwa kufuata maagizo ya kwenye skrini, ingiza jina la mtumaji kama vile jina lako la kampuni, nambari yako ya faksi.
Jina lako la mtumaji na nambari yako ya faksi inaonekana kama kichwa kwenye faksi inayotoka.
Unda mpangilio tofauti wa utambuzi wa mlio (DRD).
Huduma tofauti za mzunguko, zinazotolewa na makampuni mengi ya simu (jina la huduma hutofautiana na kampuni), hukuwezesha kuwa na nambari kadhaa za simu kwenye laini moja ya simu. Kila nambari inapewa ruwaza tifauti ya mzunguko. Unaweza kutumia nambari moja kwa simu za sauti na nyingine kwa simu za faksi. Chagua ruwaza ya mzunguo iliyopewa kwa simu za faksi katika DRD.
Kulingana na eneo, Washa na Zima huonekana kama chaguo za DRD. Chagua Washa ili utumie kipengele tofatui cha mzunguko.
Unda mpangilio wa Hali ya Kupokea.
Angalia mipangilio uliyofanya kwenye skrini iliyoonyeshwa, na kisha uendelee kwenye skrini inayofuata.
Ili kurekebisha au kubadilisha mipangilio, donoa
.
Angalia muunganisho wa faksi kwa kuteua Anza Kukagua, na kisha kuteua Chapisha ili kuchapisha ripoti inayoonyesha hali ya muunganisho.
Ikiwa kuna hitilafu zozote ambazo zimeripotiwa, fuata maelekezo yaliyo kwenye ripoti ili uzitatue.
Ikiwa skrini ya Chagua Aina ya Laini imeonyeshwa, chagua aina ya laini.
- Wakati unaunganisha kichapishi kwenye mfumo wa simu wa PBX au adapta ya taminali, teua PBX.
- Unapounganisha kichapishi kwenyue laini wastani ya simu, teua PSTN, na kisha uteue Usigundue kwenye skrini iliyoonyeshwa ya Thibitisho. Hata hivyo, kuweka hii kwa Usigundue kunaweza kusababisha printa iruke tarakimu ya kwanza ya nambari ya faksi wakati wa kudayo na itume faksi kwa nambari isiyo sahihi.