> Maelezo ya Bidhaa > Maelezo ya Programu > Programu ya Kuchapisha > Programu Inayochapisha kwa Kutumia Mbinu isiyo ya Kawaida kwenye Windows (EpsonNet Print)

Programu Inayochapisha kwa Kutumia Mbinu isiyo ya Kawaida kwenye Windows (EpsonNet Print)

EpsonNet Print ni programu ya kuchapisha kwenye mtandao wa TCP/IP. Hii inasakinishwa kutoka kwenye kisakinishi pamoja na kiendeshi cha kichapishi. Ili kuchapisha kwenye mtandao, unda lango la EpsonNet Print. Kuna vipengele na vizuizi vilivyoorodheshwa hapa chini.

  • Hali ya kichapishi inaonyeshwa juu ya skrini ya spula.

  • Ikiwa anwani ya IP ya kichapishi itabadilishwa na DHCP, kichapishi bado hugunduliwa.

  • Unaweza kutumia kichapishi kilicho kwenye sehemu tofauti ya mtandao.

  • Unaweza kuchapisha kwa kutumia mojawapo ya itifaki mbalimbali.

  • Anwani ya IPv6 haitumiki.