/ Utambazaji / Kutambaza kutoka kwa Kompyuta / Kutambaza kwa Kutumia Epson Scan 2

Kutambaza kwa Kutumia Epson Scan 2

Unaweza kuchanganua kwa kutumia kiendeshi cha kichanganuzi “Epson Scan 2”. Unaweza kuchanganua hati halisi kwa kutumia mipangilio tondoti ambayo inafaa hati za maandishi.

Angalia msaada wa Epson Scan 2 kwa ufafanuzi wa kila kipengele cha mpangilio.

  1. Weka hati halisi.

    Kumbuka:

    Ikiwa unataka kuchanganua hati kadhaa halisi, ziweke kwenye ADF.

  2. Anzisha Epson Scan 2.

  3. Weka mipangilio ifuatayo kwenye kichupo cha Mipangilio Kuu.

    • Chanzo cha Hati: Teua chanzo ambapo nakala asili inawekwa.
    • Saizi ya Hati: Teua ukubwa wa nakala asili uliyowekwa.
    • Vitufe vya / (Mwelekeo asili): Teua mwelekeo uliowekwa wa nakala asili uliyoweka. Kulingana na ukubwa wa nakala asili, kipengee hiki kinaweza kuwekwa kiotomatiki na hakiwezi kubadilishwa.
    • Aina ya Picha: Teua rangi ya kuhifadhi taswira iliyotambazwa.
    • Mwonekano: Teua mwonekano.
  4. Unda mipangilio mingine ya kutambaza ikiwezekana.

    • Unaweza kuhakiki taswira iliyotambazwa kwa kubofya kitufe cha Hakiki. Dirisha la uhakiki hufunguka, na taswira iliyohakikiwa inaonyeshwa.
      Wakati unapohakiki kwa kutumia ADF, hati halisi hutemwa kutoka kwenye ADF. Weka tena nakala asili iliyoondolewa.
    • Kwenye kichupo cha Mipangilio ya hali ya Juu, unaweza kufanya mipangilio ya kina ya marekebisho ya taswira inayofaa nyaraka za matini, kama ifuatayo.
      • Ondoa Mandhari-nyuma: Ondoa mandharinyuma ya nakala asili.
      • Uboreshaji Maandishi: Unaweza kufanya herufi hafifu kwenye nakala asili kuonekana vizuri na kolevu.
      • Sehemu ya Eneo Otomati: Unaweza kufanya herufi kuonekana vizuri na taswira kuwa laini unapofanya utambazaji wa rangi nyeusi na nyeupe kwa waraka ulio na taswira.
      • Boresha Rangi: Unaweza kuimarisha rangi iliyobainishwa kwa picha iliyotambazwa, na kisha uihifadhi kwenye kipimo cha kijivu au rangi nyeusi na nyeupe.
      • Kiwango cha juu: Unaweza kurekebisha mpaka kwa jozi ya monokromu (nyeusi na nyeupe).
      • Ugawanyaji Rangi: Unaweza kuboresha na kuimarisha mipaka ya taswira.
      • Uondoaji waa: Unaweza kuondoa ruwaza zaidi (vivuli vya wavuti) zinazoonekana wakati wa kutambaza karatasi zilizochapishwa kama vile jarida.
      • Jaza Mpaka: Unaweza kuondoa kivuli kilichotokea kwenye picha iliyotambazwa.
      • Utoaji wa Picha Mbili (Windows Pekee): Unaweza kutambaza mara moja na uhifadhi picha mbili zilizo na mipangilio tofauti ya towe kwa wakati mmoja.
    Kumbuka:

    Huenda vipengee visipatikane kulingana na mipangilio mingine uliyofanya.

  5. Weka mipangilio ya kuhifadhi faili.

    • Fomati ya Picha: Teua umbizo la kuhifadhi kutoka kwenye orodha.
      Unaweza kufanya mipangilio ya kina kwa kila umbizo la kuhifadhi isipokuwa BITMAP na PNG. Teua Chaguo kutoka kwenye orodha baada ya kuteua umbizo la kuhifadhi.
    • Jina la Faili: Thibitisha jina la kuhifadhi faili lililoonyeshwa.
      Unaweza kubadilisha mipangilio kwa jina la faili kwa kuteua Mipangilio kutoka kwenye orodha.
    • Folda: Teua kabrasha la kuhifadhi taswira iliyotambazwa kutoka kwenye orodha.
      Unaweza kuteua kabrasha jingine au uunde kabrasha jipya kwa kuteua Chagua kutoka kwenye orodha.
  6. Bofya Changanua.