/ Kutuma Faksi / Kupokea Faksi kwenye Kompyuta

Kupokea Faksi kwenye Kompyuta

Unaweza kupokea faksi na kuzihifadhi katika faili za PDF kwenye kompyuta iliyounganishwa kwenye kichapishi. FAX Utility huja na vipengele vinavyojumuisha jinsi ya kubainisha kabrasha ili kuhifadhi faksi. Sakinisha FAX Utility kabla ya kutumia kipengele hiki.

Kumbuka:

Unaweza kutumia mbinu zifuatazo ili kusakinisha FAX Utility.

  • Kutumia EPSON Software Updater (programu-tumizi ya kusasisha programu)

  • Kutumia diski iliyokuja na kichapishi chako. (Windows watumiaji Pekee)

Muhimu:
  • Ili kupokea faksi kwenye kompyuta, lazima Hali ya Kupokea kwenye paneli dhibiti ya kichapishi iwekwe kwa Otomatiki.

  • Kompyuta iliyowekwa kupokea faksi inafaa kuwashwa kila mara. Nyaraka zilizopokewa zinahifadhiwa kwa muda kwenye kumbukumbu ya kichapishi kabla ya nyaraka zilizohifadhiwa kwenye kompyuta. Ukizima kompyuta, huenda kumbukumbu ya kichapishi ikajaa kwa kuwa haiwezi kutuma nyaraka kwenye kompyuta.

  • Idadi ya nyaraka ambazo zimehifadhiwa kwa muda katika kumbukumbu ya kichapishi huonyeshwa kwenye kwenye skrini ya nyumbani.

  • Ili kusoma faksi zilizopokewa, unahitaji kusakinisha kionyeshaji cha PDF kama vile Adobe Reader kwenye kompyuta.