/ Kuhusu Mwongozo Huu / Kutumia Mwongozo Kutafuta Maelezo

Kutumia Mwongozo Kutafuta Maelezo

Mwongozo wa PDF hukuruhusu kutafuta maelezo unayotafuta kwa nenomsingi, au kuruka moja kwa moja kwa sehemu maalum kutumia maalamisho.Pia unaweza kuchapisha kurasa unazohitaji tu.Sehemu hii hufafanua jinsi ya kutumia mwongozo wa PDF ambao umefunguliwa kwenye Adobe Reader X katika kompyuta yako. Kutafuta kwa nenomsingi.

Kutafuta kwa neno msingi

Bofya Hariri > Utafutaji Mahiri.Ingiza nenomsingi (matini) kewa maelezo unayotaka kutafuta kwenye dirisha la utafutaji, na kisha ubofye Tafuta.Mipigo inaonyeshwa kama orodha.Bofya mojawapo ya mipigo iliyoonyeshwa ili kuruka hadi kwenye ukurasa huo.

Kuruka moja kwa moja kutoka kwenye maalamisho

Bofya kichwa ili kuruka kwenye ukurasa huo.Bofya + au > ili kutazama kiwango cha chini cha vichwa kwenye sehemu hiyo.Ili kurudi kwenye ukurasa wa awali, tekeleza operesheni ifuatayo kwenye kibodi yako.

  • Windows: Shikilia chini Alt, na kisha ubonyeze .

  • Mac OS: Shikilia chini kitufe cha amri, na kisha ubonyeze .

Kuchapisha kurasa unazohitaji tu

Pia unaweza kuopoa na kuchapisha kurasa unazohitaji tu.Bofya Chapisha kwenye menyu ya Faili, na kisha ubainishe kurasa unazotaka kuchapisha kwenye Kurasa kwenye Kurasa za Kuchapisha.

  • Ili kubainisha mfuatano wa kurasa, ingiza kistari ungio kati ya ukurasa wa kwanza na ukurasa wa mwisho.

    Mfano: 20–25

  • Ili kubainisha kurasa zisizo kwenye mfuatano, gawa kurasa kwa koma.

    Mfano: 5, 10, 15