/ Mipangilio ya Faksi / Kuunganisha Printa Kwenye Laini ya Simu / Kuunganisha Kifaa chako cha Simu kwenye Printa

Kuunganisha Kifaa chako cha Simu kwenye Printa

Unapotumia printa na simu yako kupitia laini moja ya simu, unganisha simu kwenye printa.

Kumbuka:
  • Ikiwa kifaa chako cha simu kina dhima ya faksi, lemaza dhina hiyo ya faksi kabla ya kuunganisha. Angalia mwongozo uliokuja na kifaa cha simu kwa maelezo.

  • Ukiunganisha mashine ya kujibu, hakikisha mpangilio wa printa wa Hutoa mlio ili Kujibu umewekwa juu zaidi ya idadi ya milio ambayo mashine yako yak ujibu imewekwa kujibu simu.

  1. Ondoa kifuniko kutoka kwa lango la EXT. upande wa nyuma wa printa.

  2. Unganisha kifaa cha simu na lango la EXT. ukitumia kebo ya simu.

    Kumbuka:

    Wakati unatumia laini moja ya simu, hakikisha umeunganisha kifaa cha simu kwenye lango la EXT. la printa. Ukigawanya laini hiyo ili uunganishe kifaa cha simu na printa kando kando, simu na printa hazitafanya kazi vizuri.

  3. Teua Faksi kwenye skrini ya nyumbani.

    Ili kuteua kipengee, tumia vitufe vya , na kisha ubonyeze kitufe cha OK.

  4. Chukua kifaa cha mkononi.

    Muunganisho umezinduliwa wakati ujumbe wa kubonyeza ili kuanza kutuma au kupokea faksi unaonyeshwa kwenye skrini.